MABONDIA KUZIPIGA SEPTEMBA 4 MWANANYAMALA

MABONDIA wa ngumi za kulipwa Ramadhan Shauri na Bakari Dunda wataoneshana
kazi katika pambano lisili la ubingwa litakalofanyika Septemba 4 mwaka huu.

Pambano hilo ambalo litakuwa la raundi nane litasindikizwa na burudani
kutoka katika kundi la \’Makhirikhiri wa bongo\’ huku likitanguliwa na
mapambano manne ya utangulizi ambapo yatafanyika katika ukumbi wa CCM
Mwinjuma wa Mwananyamala Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mratibu wa pambano hilo Ibrahim Kamwe
\’Bigright\’ alisema maandalizi ya pambano hilo yamekamilika na kuwataka wadau
wa mchezo wa ngumi kuweza kujitokeza kwa wingi ili kushuhudia mapambano
hayo.

Bigright aliyataja ambambano ya utangulizi ni kati ya Anthon Mathias na
Shabani Madilu ambapo pambano lao litakuwa la raundi sita.

Wengine ni Joseph Mbowe na Ezekiel Ezekiel raundi nne, Isa Omari na Kade
Hamis raundi sita na Sadat Miyeyusho na Herman Richard raundi sita.

Pia wamo Yona Miyeyusho na Haruna Said raundi nne, Martine Richard na
Jumanne Kilumbelumbe raundi nne na pambano la mwisho litakuwa kati ya Mwaite
Juma na Franck Pury raundi nne.

Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na huzwaji wa DVD zenye
mapambano ya mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywherth, Roy
Jones na wengine kibao.

DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye
mpambano huo na Kocha maarufu Rajabu Mhamila \’SUPER D BOXING COACH\’ hapo
na kwa Dar es Salaam DVD hizo zinapatikana katika Makutano ya Barabara ya
Uhuru na Msimbazi


Super D Boxing Coach
Photojournalist at Majira, Business Times
Email.superdboxingcoach@gmail.com