Juhudi za makusudi zatakiwa kuwawezesha wakulima wadogo

Deogratias Sarufu:

Chanzo cha mufumuko wa bei
hapa nchini ni chakula. Wataalamu
wa

uchumi wa Benki kuu ya Tanzania wanasema iwapo bei ya
chakula

itapungua, mfumuko wa bei nao hupungua. Ukweli huu
unaambatana na

ukweli mwingine kwamba taifa hili asilimia 80 ya watu wake
ni wakulima

wadogo wanaokabiliwa na changamoto nyingi zinazosababisha
kuzalisha

nafaka kidogo na hivyo kuleta uhaba wa chakula
nchini.Deogratias

Sarufu akiandika kwa niaba ya Panos East Africa anazungumzia

changamoto za mkulima wa Tanzania kwa kuangalia moja ya
mikoa

inayolisha Tanzania, Morogoro.

Kwa nchi ambayo kukua
kwa uchumi wake kunategemea zaidi uwapo wa

chakula kwa kubadili kilimo ili kifikie angalau mchango wa
asilimia 20

wa pato la taifa matumizi ya pembejeo katika kuinua ni lazima.

Mkoa wa Morogoro ni mojawapo ya mikoa ambayo inalisha
Tanzania na

umetamkwa wazi na rais Jakaya Kikwete kuwa ghala la
kuhifadhia chakula

la taifa. Mikoa mkingine ambayo inategemewa kwa nafaska ya
chakula ni

Ruvuma,Mbeya, Iringa na Rukwa.

Kutokana na umuhimu wake kwa taifa mkoa huu umeingizwa pia
katika

mpango wa kupewa vocha za pembejeo za ruzuku yaani mbolea ya
kupanda

na kukuzia na mbegu bora .

Mkoa wa morogoro ambao umebarikiwa kuwa na mabonde ya kilimo
na

umwagiliaji ,kilimo chake kwa miaka mingi kimeachwa kujiendesha

chenyewe

japo ndicho kinachotegemewa na asilimia 80 ya wananchi. Kwa
kilimo

mkoa huu bado unategemea mkulima mdogo, anayetegemea jembe
la mkono

akiwa na maarifa
kidogo au yasiyotosha kuhusu
kilimo

chenyewe.Kimsingi kilimo cha Tanzania kwa miaka mingi
kimekuwa

kikikosa teknolojia na sayansi ya kilimo yaani matumizi ya
mbolea na

viuatilifu na pia utashi kutoka kwa viongozi ulikuwa wa
kutia shaka.

Ili kukibadili kilimo cha Tanzania kama ilivyokusudiwa ipo
haja ya

kuwabadili wakulima kama alivyosema mshauri kilimo wa mkoa wa

Morogoro Bi.Aulalia Minja .

Mshauri huyo alisem a kwamba wakulima wa mkoa wake
wanakabiliwa na

changamoto kubwa ya kutekeleza agizo la Rais Kikwete kuwa
ghala la

chakula kwa kuzingatia gharama kubwa za kilimo na kipato
kidogo

kinachoambatana nacho.

Pamoja na gharama hizo kwenye pembejeo licha ya serikali
kutoa ruzuku

kw abaadhi ya wakulima, matumizi ya mbegu bora bado ni
tatizo.

“Hapa nchini matumizi ya mbegu bora ni chini ya asilimia 10 ,kiwango

ambacho ni kidogo sana ukilinganisha na nchi zingine za
Afrika.Tatizo

hilo lipo na hapa
mkoani mwangu” alisema Bi Minja.

Mkulima wa Morogoro na changamoto zake hajatofautiana na
wakulima wa

wengine wa Tanzania ambao ama hakika wanakabiliwa na
changamoto

lukuki,kama upatikanaji
wa mbegu bora .

Morogoro ambayo ni sampuli nasibu kuzungumzia wakulima wa
Tanzania

yenye zaidi ya kilomita za mraba 900,000 ni mkoa wenye kilomita za

mraba zipatazo 73,039 ambazo ni sawa na asilimia 8 ya eneo lote la

Tanzania.Kilomita hizi za mraba zinaupa sifa ya kuwa mkoa wa
pili kwa

ukubwa nchini Tanzania ukitanguliwa na Mkoa wa Tabora.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na ofisi ya mkoa wa
morogoro, mkoa

una eneo la hekta zipatazo 123,507 zinazofaa kwa kilimo.Hata
hivyo kwa

mujibu wa taarifa zilizopo mpaka sasa ni hekta 8,804 pekee ndizo

zinazotumika kwa kilimo.

Kama ilivyo kwa mikoa mingi nchini Tanzania,zaidi ya
asilimia 80 ya

wakazi wapatao 1,759,809 Mkoani humo ni wakulima.

Nikiwa Ofisi ya mshauri wa masuala ya kilimo mkoani humo,Bi
Aulalia

Minja alisema kwamba pamoja na ufinyu wa eneo linalotumika
kwa kilimo

bado kilimo hakijaleta tija inayotakiwa ambayo ingelimuondoa
mkulima

wa morogoro kutoka katika lindi la umaskini kutokana na
udhaifu katika

kilimo chenyewe kutokana na kukosekana kwa matumizi ya
kutosha ya

pembejeo na pia kuacha kutegemea mvua kwa ajili ya kilimo.

Kwa mujibu wa mshauri wa kilimo mkoa wa Morogoro Bi.Aulalia
Minja

katika msimu wa kilimo wa mwaka 2010/2011 mkoa huo ulihitaji
tani

14,198.4 za mbegu bora ikiwa ni moja ya jitihada za
kuhakikisha kuwa

mkoa unakuwa na chakula cha kutosha,lakini pia unaongeza
pato la

mkulima ili kupunguza kama sio kuondoa kabisa umasikini.

Mahitaji hayo ya mbegu bora ni kwa mazao ya

mahindi,mpunga,mtama,maharage,kunde,mbaazi, ,alizeti na
ufuta.

Hata hivyo tofauti na ilivyotarajiwa,lengo la mahitaji hayo
ya mbegu

bora halikufikiwa mkoani humo kutokana na kupatikana kiasi
kidogo cha

mbegu,ambapo kati ya tani14,198.4 za mbegu bora zilizokuwa

zikihitajika 2010/2011 ,ni tani 1,457.06 pekee za mbegu
ndizo

zilipatikana ikiwa ni takribani asilimia 1 ya mahitaji stahiki.

Afisa huyo alifafanua kuwa kiasi hicho cha mbegu bora
kilikuwa ni cha

ruzuku kwa mazao ya
mpunga na mahindi,ambapo kwa upande wa mahindi

mbegu zilizopatikana ilikuwa ni tani 1,307.06 na mpunga
ilikuwa ni

tani 150 pekee,ikiwa ni sawa na kila wilaya kupata wastani
wa tani 242

za mbegu bora.

Watu maarufu wa
uzalishaji wa mbegu za mahindi Tanseed International

Ltd,moja ya makampuni yanaozalisha mbegu bora za mahindi
aina ya Tan

250,Tan 254,Tan H611,Tan 600 na Tan222 wanasema kwamba
mahitaji kwa

sasa yanazidiwa na uzalishaji unaofanyika katika mashamba ya
mbegu!

Kwa mujibu wa maelezo ya Meneja wa Tanseed International
Ltd,Bw Isaka

Mashauri,pamoja na kutotaka kutaja kiasi cha tani
kinachozalishwa na

kampuni yake alisema pia kuwa uhaba wa mbegu unachangiwa na
gharama za

uzalishaji kuwa juu,hivyo kutoa wito kwa serikali
kuwapunguzia kodi

makampuni binafsi yanayozalisha mbegu bora ili waweze
kuzalisha mbegu

hizo kwa wingi na kukidhi mahitaji ya wakulima.

Maelezo hayo yalitoa mwanga kwamba kuna uzalishaji mdogo wa
mbegu bora

kwa kila mkulima na kufanya moja ya changamoto kubwa ya
mkulima wa

Tanzania kuwa upatikanaji wa mbegu bora.

Kwa upande wa wakulima tatizo kwao si kupatikana kwa mbegu
bali bei

kubwa ya mbegu hizo: kutokana na kuwapo kwa utata juu ya
changamoto

hasa ya wakulima kwenye mbegu bado ukweli unabaki kwamba
mkulima mdogo

hatumii mbegu bora kwa sababu tofauti japo uhaba unachangia.

Sehemu kubwa ya tatizo lake ni ughali wa mbegu na uwezo duni
wa

kununua mbegu hizo.

Wakulima wa Mikese na
Ngerengere walipozungumza na mwandishi wa

habari hizi walisema wazi kwamba changamoto inayowakabili
wao katika

suala la upatikanaji wa mbegu bora ni bei kubwa.kwa mujibu
wa wakulima

hao hata kiasi kidogo cha mbegu bora kinachopatikana
sasa,wao bado

hawezi kukipata kutokana na kuuzwa kwa bei wasiyoweza kuimudu.

Walisema kwa sasa mfuko wa mbegu bora za mahindi wenye ujazo
wa kilo 2

unauzwa kwa gharama ya shilingi za Kitanzania 4,000;ambapo
ili kuweza

kupata mbegu ya kutosha ekari moja zinahitajika kilo 6
ambazo ni sawa

na shilingi 24,000.

“Ndugu mwandishi mfuko mmoja wa mbegu bora wenye ujazo wa
kilo2

unauzwa 4,000/=na ili niweze kupanda ekari moja nahitaji
kilo 6 ambazo

ni sh 24,000 Siwezi kumudu gharama hizo,ni bora nikanunue
mbegu za

asili ambazo kwa kilo 18-20 nauziwa kwa gharama ya
6,000/=ambapo

naweza kutumia mbegu hizo kwa ekari moja” alisema mmoja wa
wakulima

Bw..Said Mchaga

Changamoto nyingine inayotajwa na wakulima hao ni baadhi ya
mbegu bora

kukosa ladha waliyoizoea,walisema kuwa baadhi ya mbegu bora
hazina

ladha nzuri ya asili waliyoizoea hasa wanapokula mahindi ya
kuchoma au

kuchemsha.

“Kusema ukweli mahindi haya ya mbegu za kisasa hayana ladha
nzuri

kabisa unapoyala yakiwa yamechomwa au kuchemsha
ukilinganisha na yale

yaliyopandwa kwa mbegu za asili.Labda kwa ugali,labda!”
alisema Bw.

Abdala Siali wa kijiji,cha Ngerengere.

Wakati mwingine unashangaa falsafa ya mkulima kuhusiana na
suala hilo

la ladha ambalo wakati mwingine linamfanya asifanye juhudi
za kutafuta

mbegu hizo bora kwa kuwa hazina ladha.

Hata hivyo wakulima
wameelezea changamoto nyine ambapo inaonekana

baadhi ya mbegu hukosa ubora wa matumizi ya kilimo.Kwa
mujibu wa afisa

ugani wa Kijiji cha Mikese,Bibi Kilonzo Mbwambo wakulima
wamekuwa

wakimwendea mara nyingi kulalamika juu ya kushindwa kuota
kwa mbegu

zilizoaminika kuwa ni bora mara baada ya kupandwa ardhini na
muda wake

wa kuota kuwadia.

Alisema kuna
uwezekano wa kuwepo kwa baadhi wafanyabiashara wasio

waaminifu wa maduka ya pembejeo za kilimo ambao huwauzia
wakulima

mbegu zilizokwisha muda wake wa matumizi ya kilimo kwa lengo
la kupata

faida kinyume na utaratibu.

“ipo sheri aya kushtaki watu hawa dawa ni kw awakulima kunua
mbegu

katika maduka ya pembvejeo wadai risiti ili kunapotoke
amushkeri

tuweze kufuatilia.” Alisema bibi shamba huyo .

Aidha alitaka wakulima kuzingatia majaribio ya uotaji wa
mbegu mpya

ambazo wanazipata kwa kuzifanyia majaribio stahiki.

Hata hivyo afisa ugani huyo alisema kuwa ili kuepukana na
tatizo hilo

huwashauri wakulima kijijini hapo kuwa na tabia ya kununua
mbegu bora

mapema na kisha kuzipanda chache kwa majaribio ili kama
hazitaota

waweze kuchukua tahadhari mapema.

Jinsi changamoto za upatikanaji wa mbegu bora mkoani humo

zilivyobainishwa na wakulima na wadau wengine,nidhahiri
kwamba wadau

wa sekta ya kilimo hususani Wizara ya kilimo,wazalishaji wa
mbegu bora

pamoja na wakulima wanatakiwa kushikamana ili kuhakikisha
kwamba mbegu

bora zinapatikana kwa wingi na kwa gharama nafuu.

Hayo yote yakifanyika jitihada za kuufanya mkoa wa Morogoro
kuwa ghala

la chakula la taifa pamoja na jitihada za kutekeleza sera ya
kilimo

kwanza yenye lengo la kutekeleza mkakati wa kukuza uchumi na
kupunguza

umasikini Tanzania (MKUKUTA) litafikiwa.

Ni wazi kuwa kunahitajika
juhudi za makusudi kwanza kubadili fikira

na kupima kw auzito unakubalika juu ya umuhimu wa mbegu bora yenye

ujazo mkubwa bila kujali ladha hasa kwa ajili ya kuongeza
kipato na

kuanzisha mfumo wa kuweka akiba ili kumudu kununua mbolea na
pembejeo

nyingine kwa ajili ya kufanya mapinduzi ya kilimo.

Katika suala la ruzuku Minja alisema kwmaba serikali
imepeleka kwa

muda unaostahili
vocha hizo japo maeneo mengtine ya mkoa wa Morogoro

walanguzi wametokea na kuvuruga mfumo kwa kuwarubuni wa
kulima.

“Wapo wakulima kama katika eneo la mvomero na pia kilosa
wamekuwa

wakipewa fedha kidogo na kuuza vocha hizo hali ambayo
inaleta shida na

kuchelewesha mabadiliko miongoni mwa wakuloima wetu.”
Alisema Minja.

Morogoro ambayo ni miongoni mwa mikoa kadhaa inayopewa
ruzuku ya

pembejeo imekuw aikikabiliw ana ufiosadi wa ajabu wa
matumizi mabaya

ambapo wakulima wandanganywa kukubali shilingi cache kwa
kutoa hatiz a

ununuzi wa pembejeo kumbe hawakununua na hivyo mashamba
kukosa mblea

inayohitajika na mbegu zinaozstahili.

Kwa hiyo tatizo si mbegu tu na fikira zao bali pia na
Mawakala ambao

kwa kushirikiana na viongozi wengine wasiokuwa waaminifu
wamekuwa

wakijilipa vocha bila kutoa huduma.

Mawakala wamekuwa hodari mno kubuni mbinu ya kulaghaia
wakulima

maskini na kuwafanya wakubaliane nao, wakidhani wanapata
kumbe wamepatikana.

Vocha ya ruzuku katika pembejeo ni mkombozi kwa jamii , angalau kama

sehemu ya kilimo darasa na pia kuwezesha wakulima maskini
lakini kwa

mtindo wa ulaghai unaojitokeza inakuwa taabu kubwa kubadili
maisha ya

wakulima.

“Kuna tatizo la mawakala kuweka bei ya juu sana ya
mbolea na hata

mbegu” alisema mmoja wa wakulima Madenge na kuongeza
kwamba kutokana

na hali hiyo ni vyema
mawakala wakabanwa na kuwa na mtazamo sawa na

serikali wa kusaidia wakulima kuondokana na umaskini.

mwisho